
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa huru na hadithi kutoka SBS Audio, zinazokuunganisha na maisha nchini Australia na Waaustralia wanaozungumza Kiswahili. Kipindi hiki kinatoa habari za kujitegemea na hadithi za kuvutia kwa jamii ya Waswahili nchini Australia.
Episodes

Taarifa ya Habari:Ripoti mpya yaitaka Australia iboreshe usalama wa dawa na itoe wakalimani kwa jamii za tamaduni mbalimbali
Ripoti mpya imeangazia changamoto kubwa za usalama wa dawa zinazowakabili Waaustralia wenye tamaduni mbalimbali, na inatoa wito wa upatikanaji mkubwa wa taarifa na wakalimani wa dawa zinazotumia lugha nyingi.

Yaliyojiri Afrika:7 wafariki katika ajali ya helikopta Kenya
Watu saba, wakiwemo raia watano wa Marekani na mkuu wa ujasusi wa Ecuador, wamefariki baada ya helikopta ya watalii kuanguka karibu na Mlima Ololokwe, katika kaunti ya Samburu nchini Kenya.

Makala Leo:Mabadiliko ya NDIS yatakuathiri vipi?
Mamia ya maelfu ya watu watapoteza msaada kutoka NDIS, baada ya mabadiliko yanayolenga kupunguza ukuaji katika mpango huo kupitishwa ndani ya Seneti kwa uungwaji mkono wa Upinzani wa Mseto usiku wakuamkia.

Yaliyojiri Afrika:Askari pori watuhumiwa kwa mauaji ya raia Tanzania
Kituo cha sheria cha haki za binadamu Tanzania, kime eleza wasiwasi kuhusu madai ya watu kuuawa, kujeruhiwa au kupotea katika maeneo ya hifadhi nchini humo.

Taarifa ya Habari:Upinzani wa Mseto watishia kuzuia mabadiliko ya NDIS isipokuwa mwanya wa kodi ya mjane utakapofungwa
Upinzani wa Mseto unatishia kuzuia mabadiliko ya serikali kwa NDIS, isipokuwa serikali ya Labor iharakishe sheria ya kufunga kile kinachoitwa kodi ya mjane.

Makala Leo:Mageuzi ya NDIS yanatarajiwa kuwa sheria ila, wanaharakati wadai makato yata sababisha madhara
Mageuzi ya Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Watu Wenye Ulemavu yamejadiliwa katika Seneti, huku sheria ikitarajiwa kupitishwa wiki hii kwa msaada wa Upinzani wa Mseto.

Can you pick fruit from someone's garden? - Australia Yafafanuliwa:Je, unaweza chuma matunda kutoka bustani ya mtu?
Walking through an Australian suburb, you might spot everything from curry leaves and lemons to tomatoes and herbs growing in front gardens or on verges. But is it legal to pick it? This guide explains when it's legal to pick produce, why permission matters, and how community gardens offer another way to grow your own food. - Ukitembea katika kitongoji cha Australia, unaweza ona kila kitu kuanzia

Taarifa ya Habari:Wafanyakazi wa kusambaza vyakula kuongezewa mshahara kuanzia leo
Takriban idadi yawa Australia 250,000 wanaosafirisha vyakula kutoka hotelini na dukani kwa ajili ya kujikimu, wanatarajiwa kupokea mshahara wa chini kisheria kwa mara ya kwanza.

Makala Leo:Serikali kuwekeza mamilioni katika nyumba za waathiriwa wa unyanyasaji wa majumbani; lakini je, inatosha?
Mgogoro wa makazi ukiendelea, vurugu za kifamilia na majumbani (DFSV) ndio sababu kuu ya wanawake na watoto kuondoka nyumbani kwao na kukosa makazi.

SBS Learn Eng Ep 117 Jinsi yakuzungumza kuhusu kukopa vitabu
Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kukopa vitabu katika maktaba?

Taarifa ya Habari:Ripoti ya mwisho kuhusu mabadiliko yaliyopendekezwa na Serikali kwa Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Ulemavu itawasilishwa Bungeni
Ripoti ya mwisho kuhusu mabadiliko yaliyopendekezwa na Serikali kwa Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Ulemavu itawasilishwa Bungeni leo. Uchunguzi huo ulizinduliwa katika mwezi Mei ili kuchunguza mapendekezo ya Serikali, ya kuokoa karibu dola bilioni 38 kwa kipindi cha miaka minne.

Yaliyojiri Afrika: Uganda na Tanzania za zindua ushirikiano wa nishati
Bandari ya Tanga itakuwa kitovu muhimu cha nishati katika jumuiya ya Afrika Mashariki, chini ya ushirikiano mpya wa nishati uliozinduliwa kati ya serikali ya Uganda na Tanzania.

Makala Leo:Sensa imekwisha ila, bado hauja chelewa kama hauja jaza fomu yako
Sensa ya 2026 imekwisha na idadi kubwa ya Waaustralia walikamilisha utafiti huo mtandaoni.

Taarifa ya Habari:Serikali yawahakikishia watu kwamba Sensa itakuwa salama
Serikali inawahakikishia watu kwamba Sensa itakuwa salama, kufuatia visa vya hivi karibuni vya roboti za AI kufanya ujambazi na uvunjaji wa data katika mashirika makubwa.

Yaliyojiri Afrika:Wanariadha wa Uganda watoweka Scotland
Mabondia wanne wa timu ya Uganda, wametoweka baada yakufeli kujitokeza kwa safari zao za ndege zakurejea nyumbani, baada ya kushiriki katika michezo ya jumuiya yamadola mjini Glasgow.

Makala Leo: Watetezi wa ulemavu waomba mlinzi nakuonya kuhusu 'athari kubwa' mageuzi yanapokaribia
Watetezi wa ulemavu wanaihimiza serikali kufikiria upya mabadiliko ya Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Ulemavu unao julikana kama NDIS, kabla ya kura ya bunge inayokaribia kuhusu mageuzi yaliyopendekezwa.

Taarifa ya Habari:Wafanya biashara waomba ushirikiano na serikali kabla ifanye mabadiliko katika uhamiaji
Vikundi vya wafanyabiashara vinaihimiza serikali ya shirikisho kushirikiana nao, katika mashauriano kabla ya mabadiliko yoyote makubwa kutangazwa kuhusu sera ya uhamiaji.

Taarifa ya Habari:Ofisi ya takwimu ya Australia yahimiza wanao ishi katika nyumba zenye watu wengi wasiwe na hofu kushiriki katika sensa
Usiku wa sensa ukikaribia, maafisa wa Ofisi ya Takwimu ya Australia wanawahimiza watu wanao ishi katika makaazi yenye watu wengi sana, wasiwe na hofu yakushiriki kwa sababu hapatakuwa athari yoyote ya kisheria.

What are my rights if stopped by police in Australia? - Australia Yafafanuliwa:Haki zangu ni zipi kama nitasimamishwa na polisi nchini Australia?
Police officers have a range of operational powers they can exercise under legislation, including to ask questions, give ‘move on’ directions and conduct searches. Here’s what you need to know about your basic rights and obligations in a police interaction. - Maafisa wa jeshi la polisi wana mamlaka mbalimbali ya kiutendaji ambayo wanaweza kuyatumia chini ya sheria, ikiwa ni pamoja na kuuliza maswa

SBS Learn Eng Ep 116 Jinsi yakuzungumza kuhusu kumtembelea daktari wa wanyama
Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kumtembelea daktari wa wanyama?

Taarifa ya Habari:Mfanyabiashara afariki mjini Melbourne baada ya tukio linalo shukiwa kutekelezwa na wezi
Mfanyabiashara mmoja wa duka mjini Melbourne amefariki baada ya kushambuliwa alipokuwa akijaribu kuzuia kundi la vijana walio kuwa waki iba dukani.

Yaliyojiri Afrika: DRC yaadhimisha GENOCOST
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Félix Tshisekedi, ameongoza kumbukumbuku ya mauaji ya GENOCOST jijini Kinshasa, inayofanyika kila tarehe 2 mwezi Agosti.

Taarifa ya Habari:Mamia ya watu wakimbia mapigano Tigray na kuingia Sudan
Mamia yawa Ethiopia kutoka eneo la kaskazini mwa Tigray, wamevuka mpaka na kuingia nchi jirani ya Sudan katika siku mbili zilizopita, wakikimbia mapigano karibu na mpaka.

Makala Leo:Australia inakabiliwa na 'tsunami ya uharibifu' mkubwa kutokana na mlipuko wa virusi vya homa ya ndege H5
Jimbo la Kusini Australia huenda linakabiliwa na tukio la kwanza la vifo vingi vya wanyamapori nchini Australia linalohusishwa na homa ya ndege ya H5N1.

Makala Leo:Benki ya Hifadhi yasema wa Australia wengi hawa elewi jinsi viwango vya riba vinavyofanya kazi
Kiwango cha mfumuko wa bei nchini Australia kimepungua, lakini shinikizo la bei la msingi linabaki kuwa juu sana.

Taarifa ya Habari
Mdhibiti wa ushindani [[ACCC]] ameombwa na serikali ya shirikisho kufuatilia vituo vya mafuta kwa matukio yoyote ya kupunguzwa kwa bei - sasa kwa kuwa punguzo la muda la ushuru wa mafuta limeisha.Visa 74 vya aina ya H-5 ya homa ya ndege vimethibitishwa nchini Australia.Hiyo inajumuisha uthibitisho wa tukio la kwanza la vifo vingi humu nchini kutokana na virusi hivyo Kusini mwa Australia.Mji wa Ceu

Taarifa ya Habari:Kiongozi wa Victoria, ajiuzulu baada ya siku kadhaa za shinikizo dhidi ya uongozi wake
Jacinta Allan amejiuzulu kama Kiongozi wa Victoria, akisema ni uamuzi sahihi kwa Wa-Victoria. Tangazo hilo limekuja nusu saa tu baada ya changamoto inayotarajiwa ya uongozi katika mkutano uliopangwa wa chama cha wabunge, kuashiria kurudi kwa bunge la jimbo.

Australia Yafafanuliwa:Tamasha ya Garma ni nini, na kwa nini ni muhimu?
Kila mwaka, maelfu ya watu husafiri kwenda katika jamii ya kijijini kaskazini mashariki mwa Arnhem Land katika Eneo la Kaskazini.

Makala Leo: Jacinta Allan akataa kujiuzulu, pambano la uongozi wa chama cha Labor cha Victoria likiongezeka kasi
Kiongozi wa Jimbo la Victoria, Jacinta Allan, anasema atapambana na changamoto ya uongozi inayokuja baada ya viongozi wa mirengo tafuati ndani ya chama cha Labor, kukutana na kukubaliana kwamba amepoteza uungwaji mkono wa wengi katika mkutano wao.

Taarifa ya Habari: Kiongozi wa Victoria asisitiza hajiuzulu!
Kiongozi wa jimbo la Victoria, Jacinta Allan, anasema hatajiuzulu kutoka wadhifa wake, miezi minne kabla ya uchaguzi wa jimbo hilo.

Yaliyojiri Afrika:Kenya yapokea tani 4.5 zavifaa vya matibabu vya Ebola kutoka India
Kenya imepokea shehena ya kwanza ya tani 4.5 za vifaa vya matibabu kutoka kwa serikali ya India, ili kuimarisha uwezo wa nchi kujiandaa kukabiliana na uwezekano wa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

Taarifa ya Habari: Hatua ya Marekani kuongeza ushuru kwa mauzo ya nje ya Australia yazua ukosoaji
Utawala wa Trump umeongeza ushuru kwa mauzo ya nje ya Australia kutoka asilimia 10 hadi 12.5, huku kiwango kipya kikianza kutumika alasiri ya leo Ijumaa.

Makala Leo:Nini cha kutarajia kutoka kwa mfumo mpya wa tahadhari ya dharura wa Australia
Australia inajiandaa kuanzisha mfumo mpya wa kitaifa wa tahadhari ya dharura, ulioundwa kutoa tahadhari muhimu haraka na kwa uhakika zaidi wakati wa majanga.

Makala Leo:China yaambia Australia iache kuzungumzia Bahari ya Kusini mwa China wakati mvutano ukiongezeka katika Mkutano wa ASEAN
Mkutano wa Kikanda wa ASEAN unakamilika mjini Manila, ambapo Australia imeibua wasiwasi kuhusu hatua za kijeshi za China katika eneo hilo.

Taarifa ya Habari:Waziri Mkuu ataka chama cha Labor, kijitolee kupunguza shinikizo za gharama ya maisha
Waziri Mkuu Anthony Albanese, amesisitiza kujitolea kwa chama chake kupunguza shinikizo la gharama la maisha katika mkutano wa kitaifa wa chama tawala.

Yaliyojiri Afrika:Kituo chakujitenga cha Ebola nchini Kenya cha wapokea wamarekani 7 kutoka DRC
Wahudumu7 wamisaada kutoka wamarekani walikuowa wakisaida kupambana na Ebola DRC, wamewekwa katika kituo cha karantini nchini Kenya.

SBS Learn Eng Ep 115 Jinsi yakuzungumza kuhusu kufanya kazi ya ziada
Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kufanya kazi ya ziada?

Taarifa ya Habari:Waziri Wong aelekea katika kongamano lamawaziri wa mambo ya nje wa ASEAN kuimarisha uhusiano wa Australia na nchi wanachama
Waziri wa Mambo ya Nje Penny Wong anatarajiwa kwenda Ufilipino kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Asia Mashariki na Jukwaa la Kikanda la ASEAN.Tume ya Dhamana na Uwekezaji ya Australia inasema imepata rekodi ya dola milioni 830 katika amri za adhabu za kiraia wakati wa Mwaka wa Fedha wa 2025-2026. Tume hiyo ilianzisha chunguzi zaidi ya 250, ambazo zilisababisha hatia 25 za jinai na

Australia Yafafanuliwa:Kijana wangu anaweza anza kufanya kazi lini nchini Australia?
Kuanza kazi ya muda mfupi kunaweza kuwa uzoefu wenye maana kwa kijana, kuongeza kujithamini kwake, kumsaidia kujifunza ujuzi mpya na kupata pesa zake za kwanza.

Makala Leo:Mazoezi muhimu yakimataifa yajeshi yaanza katika Wilaya ya Kaskazini
Zoezi kubwa zaidi la kimataifa la Jeshi la Anga la Australia, linaendelea katika Eneo la Kaskazini na litafanyika kwa wiki tatu zijazo.

Taarifa ya Habari:Greens wataka makampuni ya mawasiliano nchini kutoa huduma yakuaminika kwa wateja
Chama cha Greens kinatoa wito wa mageuzi ambayo kisheria yatahitaji kampuni zama wasiliano kama Telstra, Optus na Vodafone kutoa huduma ya kuaminika kwa wateja.

Makala Leo: Mitandao ya teknolojia yaambiwa irekebishe pengo za ulaghai wakujamiana
Kamishna wa Usalama Mtandaoni wa Australia anatoa tahadhari kuhusu ulaghai wa kingono mtandaoni, baada ya kupokea malalamiko zaidi ya 2,000 katika miezi sita tu.

Taarifa ya Habari:Watoto wa Australia kuanza kuamua katika shule ya msingi kama watafuata taaluma za sayansi na teknolojia kwa msaada wa wazazi
Utafiti mpya unaonyesha kuwa watoto wa Australia wanaweza kuanza kuamua katika shule ya msingi kama watafuata taaluma za sayansi na teknolojia wanapokuwa wakubwa, huku wazazi wakiwa na ushawishi zaidi kuliko walimu katika maamuzi hayo.

Makala Leo: Argentina na Uhispania zaishi ndoto zakipekee za Kombe la Dunia
Argentina na Uhispania wanaishi ndoto ya kipekee ya Kombe la Dunia, baada yakutinga fainali ya kombe hilo. Mjini Buenos Aires na Madrid, mashabiki wanachangia jinsi walivyopitia tamthilia, hisia na sherehe.

Taarifa ya Habari:Ombi latolewa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na wakaazi wa Torres Strait
Kuna wito wa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na watu kutoka Visiwa vya Torres Strait, huku vikao vikiendelea katika uchunguzi wa ubaguzi wa rangi wa Serikali ya Shirikisho huko Darwin.

Makala Leo:Ufaransa na Uhispania tayari kwa pambano la nusu fainali
Nusu fainali za Kombe la Dunia zimewadia, Ufaransa na Uhispania zikijiandaa kufufua moja ya ushindani mkubwa wa soka la kimataifa. Tunaangalia kwa karibu habari za hivi punde za timu hizo na kusikia kutoka kwa kambi zote mbili kabla ya pambano kubwa la kesho.

Taarifa ya Habari:Vyuo vikuu kukabiliwa na faini kubwa vikishindwa kupambana na ubaguzi wa rangi
Serikali ya Shirikisho inasema vyuo vikuu vinaweza kukabiliwa na faini ikiwa vitashindwa kupambana na ubaguzi wa rangi chini ya viwango vipya vilivyoanzishwa Jumatatu 13 Julai 2026.

Makala Leo:Kusini Australia yatoa mpango wakupiga marufuku wahalifu wa vurugu kutoka programu zakuchumbiana
Jimbo la Kusini Australia limefichua mpango wa kwanza wa kupiga marufuku vurugu za majumbani na wahalifu wa kujamiana kutoka kwa programu za kuchumbiana.

Makala Leo:Mashambulizi mapya yashuhudiwa Iran na Marekani zikibishana kuhusu kufunguliwa kwa Hormuz
Marekani na Iran zimebadilishana wimbi jingine la mashambulizi, huku mapigano yakiongezeka kuhusu Mlango-Bahari wa Hormuz yakisukuma makubaliano ya kidiplomasia ya mwezi uliopita karibu kuvunjika.

Taarifa ya Habari:Daglo na maafisa wengine wa RSF wahukumiwa adhabu ya kifo
Mahakama ya Kupambana na Ugaidi na Makosa Dhidi ya Taifa iliyoko mjini Port Sudan nchini Sudan, , imemhukumu kifo kiongozi wa kundi la wanamgambo wa RSF, Mohamed Hamdan Daglo pamoja na maafisa wengine 15 wa RSF.

Yaliyojiri Afrika: Usalama waimarishwa katika mitaa ya Tanzania
Usalama unaendelea kuimarishwa katika miji mikubwa ya Tanzania, maafisa wa Polisi na Jeshi wenye silaha wakifanya doria.

Mbappé aiweka Ufaransa katika nusu fainali
Ufaransa imetinga nusu fainali ya Kombe la Dunia, baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Morocco. Kylian Mbappé amefunga mabao nane sawa na Lionel Messi, wakati Ousmane Dembélé akikamilisha ushindi huo.

Taarifa ya Habari:Polisi wachunguza kama kifo katika jimbo la Kusini Australia, kina husishwa na kupotea kwa huduma za Telstra Jumatano
Polisi wanachunguza kama kifo kinahusishwa na kupotezwa kwa huduma ya Telstra kote nchini Jumatano. Wapelelezi wa Kusini Australia wamethibitisha mtu mmoja alifariki katika hospitali ya kanda Jumatano, lakini polisi hawakuwa wamearifiwa kuhusu kifo hicho.

Australia Yafafanuliwa: Sensa ya 2026: Unacho stahili jua kuhakikisha una hesabiwa
Sensa ya 2026 itafanyika Jumanne tarehe 11 Agosti na kila mtu nchini Australia usiku huu lazima ahesabiwe.

Makala Leo: Waziri Mkuu Albanese aendeleza msukumo wake wakidiplomasia katika Pasifiki
Waziri Mkuu Anthony Albanese ameweka ratiba kabambe ya mkataba mpya kamili na Visiwa vya Solomon, akisema angependa kuuona ukikamilika mwishoni mwa mwaka huu.

Taarifa ya Habari:Unyanyasaji wa kingono unaendelea kutumiwa kama silaha ya kivita DRC
Mamlaka katika jimbo la Kusini Australia, zimethibitisha kisa cha pili cha homa ya ndege aina ya H5 katika jimbo hilo.

Chiry"wasichana wenzangu njooni tuboreshe afya zetu kupitia mpira"
Jamii ya wakenya wanao ishi mjini Sydney, NSW walishuhudia historia ikiandikwa jioni ya Jumapili 28 Juni 2026 timu mpya ya mpira wa miguu ya kina dada ilipo cheza mechi yao ya kwanza katika uwanja wa Rydalmere.

Uhispania na Ubelgiji za tinga robo fainali wakati Ronaldo aaga Kombe la Dunia
Uhispania na Ubelgiji zimefuzu kwa robo fainali, wakati ndoto za Kombe la Dunia za wenyeji Marekani na Ureno ya Cristiano Ronaldo ziki gonga miamba.

Taarifa ya Habari:Ofisi ya Takwimu ya Australia yazindua kampeni ya tamaduni mbalimbali kabla ya Sensa ya mwezi ujao
Ofisi ya Takwimu ya Australia imezindua kampeni ya tamaduni mbalimbali kabla ya Sensa ya mwezi ujao, ikijumuisha matangazo katika lugha 28 tofauti.

Makala Leo: Wiki ya NAIDOC ni nini, na nini kimejificha nyuma ya kauli mbiu ya mwaka huu?
Maadhimisho ya Wiki ya NAIDOC ya Kitaifa yanafanyika kote nchini Australia wiki hii, kwa ajili ya kusherehekea na kutambua historia, utamaduni na mafanikio ya watu wa Asili na wakaazi wa Visiwa vya Torres Strait.

Makala Leo: Makampuni makubwa ya mtandao wakijamii yatetea sera zao mbele ya Tume ya Kifalme
Kampuni kubwa ya mtandao ya kijamii, Meta, ilifika mbele ya Tume ya Kifalme kuhusu Unyanyasaji wa Wayahudi na Uwiano wa Kijamii jana Julai 6, ikitetea rekodi yake ya kukomesha matumizi mabaya mtandaoni.

Taarifa ya Habari:Tiba ya majaribio ya Ebola yazinduliwa Mashariki mwa DR Congo
Raia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamepata matumaini mapya baada ya kuanza kwa majaribio ya dawa mbili zinazolenga kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

SBS Learn Eng Ep 114 Jinsi yakuzungumza kuhusu Sensa na usalama wa data
Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu Sensa na usalama wa data?

Yaliyojiri Afrika:Mvutano wakidiplomasia waiubuka kati ya Ghana, Nigeria na Afrika Kusini
Nigeria imesema itaitaka Afrika Kusini ilipe fidia kwa raia wake acha mali na biashara zao baada yaku kimbia nchi hiyo kutoka na maandamano dhidi ya wahamiaji.

Mtao "Ukosefu wa utulivu wa kiakili na usimamizi mubovu wa mchezo umezigharimu timu za Afrika"
Mashabiki wa timu za Afrika katika Kombe la Dunia la FIFA 2026, walipata pigo kubwa katika siku ya 20 na 21 ya michuano hiyo.

Taarifa ya Habari:Serikali ya shirikisho yaongeza gharama ya maombi kwa vitengo kadhaa vya visa za Australia kwa asilimia 25
Ada ya maombi ya visa ya mwanafunzi imeongezeka tangu Julai 1 kutoka $2,000 hadi $2,500, huku Visa ya Muda ya Uzamili, au visa nambari 485, sasa inagharimu $5,750.

Ureno yavunja mioyo yawa Kroeshia wakati Uhispania yatinga raundi ya 16
Katika Siku ya 22 ya Kombe la Dunia la FIFA, Ureno iliwashinda Kroeshia katika mechi ya mwisho ya Kombe la Dunia ya Luka Modrić, Uhispania ili icharaza Austria, na Uswisi ikaishinda Algeria na kufuzu kwa Raundi ya 16.

'Elimu kama chombo cha matumaini': Mwanafunzi mkimbizi Alina kuhusu kujenga upya maisha yake nchini Australia
Wanafunzi wakimbizi wanajenga upya maisha yao nchini Australia kupitia mpango mpya wa majaribio ya makazi, unaounganisha masomo yao ya chuo kikuu na viwanda ambapo kuna uhaba mkubwa wa wafanyakazi kama vile uuguzi.

Taarifa ya Habari: Wanafunzi wanane washitakiwa kwa mauaji Kenya
Polisi wamewakamata vijana wawili baada ya mvulana wa miaka 15 kuachwa afe nje ya kituo cha matibabu cha jamii mjini Melbourne.

DR Congo yawapa mamilioni fahari
Mwaka huu DR Congo ilimaliza ukame wakuto shiriki katika Kombe la Dunia la FIFA baada ya zaidi ya miaka 50.

Taarifa ya Habari: Mamilioni ya Waustralia kuamka kesho Julai 1 kwa mishahara ya juu na kodi ya chini ya mapato
Bei ya petroli imeshuka hadi viwango ambavyo havijaonekana tangu mwanzo wa 2022. Taasisi ya Petroli ya Australia inasema wastani wa kitaifa wa lita moja ya mafuta yasiyo na risasi ulishuka zaidi ya senti 6 wiki iliyopita - hadi chini kidogo ya dola 1.60.

Wajerumani na Waholanzi watupwa nje ya Kombe la Dunia 2026
Siku ya 19 ya Kombe la Dunia la FIFA ilijumuisha mechi tatu za mchujo zenye ushindani mkali, huku Ujerumani na Uholanzi zikiondolewa baada ya mikwaju ya penati, wakati huo huo Brazil ilinyakua ushindi katika mechi yao muda mfupi kabla ya kipenga cha mwisho.

Australia Yafafanuliwa: Jinsi yakujiunga na soka jumuishi nchini Australia
Sio kutia chumvi tunaposikia kwamba Kombe la Dunia la FIFA lina tarajiwa kuleta dunia pamoja katika mwezi wa Juni. Baada ya yote, mpira wa miguu unajulikana kama mchezo maarufu zaidi duniani.

Taarifa ya Habari: Mkuu wa jeshi azuia shughuli za Nation Media Group nchini Uganda
Shirika kubwa zaidi huru la habari nchini Uganda Nation media group limearifu kuwa limewekwa chini ya ulinzi mkali wa kijeshi mapema Jumapili.

Baranga"nakaribisha wanaume wote katika kongamano maalum, tujadili maswala muhimu kwetu"
Wanaume kutoka jumuiya za Afrika Mashariki wanao ishi jimboni New South Wales, wana jiandaa kwa kongamano maalum Jumamosi 27 Juni 2026.

Taarifa ya Habari:"Sheria tata za mageuzi ya kodi zitawafaidi watu wengi" asema Mweka Hazina wa Shirikisho
Mweka Hazina wa Shirikisho Jim Chalmers anasema wafanyakazi, wanunuzi wa nyumba za kwanza na vizazi vijavyo watafaidika na sheria zenye utata za mageuzi ya kodi ambazo zimepitishwa hivi karibuni bungeni.Polisi warusha mabomu ya kutoa machozi dhidi ya waandamanaji katika maeneo mbalimbali mjini Nairobi huku makundi yanayoongozwa na vijana yakikumbuka miaka miwili tangu maandamano ya Gen Z. Watu kad

Australia yatinga raundi ya 32 baada ya sare yakutofungana dhidi ya Paraguayi
Socceroos wamefanikiwa kufika hatua ya mchujo baada ya kupata sare yakutofungana katika Kundi D, wakati Ecuador ikiwaacha wajerumani vinywa wazi katika Kundi E na kufuzu kushiriki katika hatua ya timu bora 32.

Australia Yafafanuliwa:Bendera ya watu wa Visiwa vya Torres Strait:Ardhi,Bahari na Watu
Nchini Australia, unaweza ona bendera tatu zikipeperushwa pamoja: Bendera ya Taifa ya Australia, Bendera ya Waaborijini na Bendera ya Watu wa visiwa vya Torres Strait.

Taarifa ya Habari:Maelfu wahofiwa wamefariki baada ya tetemeko kubwa la ardhi katika mji mkuu wa Venezuela
Hali ya dharura ime anza kutumika nchini Venezuela baada ya matetemeko mawili makubwa ya ardhi, yaliyotokea magharibi mwa mji mkuu wa Caracas, na kuua watu wasiopungua 32 pamoja nakuwajeruhi mamia.

Can nature help tackle loneliness? - SBS Examines: Je, mazingira ya asili yanaweza kabili upweke?
In a recent study of LGBTQIA+ asylum seekers and refugees, nature was used not just as a meeting place, but as an environment where participants felt safe without being questioned or judged. - Katika utafiti wa hivi karibuni wa waomba hifadhi na wakimbizi wa LGBTQIA+, mazingira yaki asili hayakutumika tu kama mahali pa kukutania, bali kama mazingira ambapo washiriki walihisi salama bila kuhojiwa a











